< Zaburi 92 >

1 Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
מזמור שיר ליום השבת טוב להדות ליהוה ולזמר לשמך עליון׃
2 kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
להגיד בבקר חסדך ואמונתך בלילות׃
3 kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
עלי עשור ועלי נבל עלי הגיון בכנור׃
4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
כי שמחתני יהוה בפעלך במעשי ידיך ארנן׃
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
מה גדלו מעשיך יהוה מאד עמקו מחשבתיך׃
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
איש בער לא ידע וכסיל לא יבין את זאת׃
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
בפרח רשעים כמו עשב ויציצו כל פעלי און להשמדם עדי עד׃
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
ואתה מרום לעלם יהוה׃
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
כי הנה איביך יהוה כי הנה איביך יאבדו יתפרדו כל פעלי און׃
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
ותרם כראים קרני בלתי בשמן רענן׃
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
ותבט עיני בשורי בקמים עלי מרעים תשמענה אזני׃
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
צדיק כתמר יפרח כארז בלבנון ישגה׃
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
שתולים בבית יהוה בחצרות אלהינו יפריחו׃
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
עוד ינובון בשיבה דשנים ורעננים יהיו׃
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
להגיד כי ישר יהוה צורי ולא עלתה בו׃

< Zaburi 92 >