< Zaburi 91 >
1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Aquelle que habita no esconderijo do Altissimo, á sombra do Omnipotente descançará.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
Direi do Senhor: Elle é o meu Deus, o meu refugio, a minha fortaleza, e n'elle confiarei.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
Porque elle te livrará do laço do passarinheiro, e da peste perniciosa.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Elle te cobrirá com as suas pennas, e debaixo das suas azas te confiarás: a sua verdade será o teu escudo e rodella.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Não terás medo do terror de noite nem da setta que vôa de dia,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Nem da peste que anda na escuridão, nem da mortandade que assola ao meio-dia.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Mil cairão ao teu lado, e dez mil á tua direita, mas não chegará a ti.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Sómente com os teus olhos contemplarás, e verás a recompensa dos impios.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Porque tu, ó Senhor, és o meu refugio: no Altissimo fizeste a tua habitação.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Nenhum mal te succederá, nem praga alguma chegará á tua tenda.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
Porque aos seus anjos dará ordem a teu respeito para te guardarem em todos os teus caminhos.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
Elles te sustentarão nas suas mãos, para que não tropeces com o teu pé em pedra.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Pisarás o leão e a cobra; calcarás aos pés o filho do leão e o dragão.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Porquanto tão encarecidamente me amou, tambem eu o livrarei; pôl-o-hei em retiro alto, porque conheceu o meu nome.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Elle me invocará, e eu lhe responderei; estarei com elle na angustia; d'ella o retirarei, e o glorificarei.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Fartal-o-hei com longura de dias, e lhe mostrarei a minha salvação.