< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
ישב בסתר עליון בצל שדי יתלונן
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
אמר--ליהוה מחסי ומצודתי אלהי אבטח-בו
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
כי הוא יצילך מפח יקוש מדבר הוות
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
באברתו יסך לך--ותחת-כנפיו תחסה צנה וסחרה אמתו
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
לא-תירא מפחד לילה מחץ יעוף יומם
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
מדבר באפל יהלך מקטב ישוד צהרים
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
יפל מצדך אלף--ורבבה מימינך אליך לא יגש
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
רק בעיניך תביט ושלמת רשעים תראה
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
כי-אתה יהוה מחסי עליון שמת מעונך
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
לא-תאנה אליך רעה ונגע לא-יקרב באהלך
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
כי מלאכיו יצוה-לך לשמרך בכל-דרכיך
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
על-כפים ישאונך פן-תגף באבן רגלך
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
על-שחל ופתן תדרך תרמס כפיר ותנין
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
כי בי חשק ואפלטהו אשגבהו כי-ידע שמי
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
יקראני ואענהו--עמו-אנכי בצרה אחלצהו ואכבדהו
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
ארך ימים אשביעהו ואראהו בישועתי

< Zaburi 91 >