< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Wer da wohnt im Schirm des Höchsten und im Schatten des Allmächtigen weilt,
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
der spricht zum HERRN: »Meine Zuflucht und meine Burg, mein Gott, auf den ich vertraue!«
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
Denn er ist’s, der dich rettet aus den Voglers Schlinge, von der unheilvollen Pest.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Mit seinen Fittichen deckt er dich, und unter seinen Flügeln bist du geborgen, Schild und Panzer ist seine Treue.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Du brauchst dich nicht zu fürchten vor nächtlichem Schrecken, vor dem Pfeil, der bei Tage daherfliegt,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
nicht vor der Pest, die im Finstern schleicht, vor der Seuche, die mittags wütet.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Ob tausend dir zur Seite fallen, zehntausend zu deiner Rechten: an dich kommt’s nicht heran;
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
nein, lediglich mit eignen Augen wirst du’s schauen und zusehn, wie den Frevlern vergolten wird.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Ja, du, o HERR, bist meine Zuflucht: den Höchsten hast du zum Schutz dir erwählt.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Kein Übel wird dir begegnen, kein Unheilsschlag deinem Zelte nahn;
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
denn seine Engel wird er für dich entbieten, daß sie dich behüten auf all deinen Wegen;
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
auf den Armen werden sie dich tragen, damit dein Fuß nicht stoße an einen Stein;
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
über Löwen und Ottern wirst du schreiten, wirst junge Löwen und Schlangen zertreten.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
»Weil er fest an mir hängt, so will ich ihn retten, will ihn schützen, denn er kennt meinen Namen.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Ruft er mich an, so will ich ihn erhören; ich steh’ ihm bei in der Not, will frei ihn machen und geehrt.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Mit langem Leben will ich ihn sättigen und lasse ihn schauen mein Heil.«

< Zaburi 91 >