< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Celui qui habite dans la retraite du Très-Haut Repose à l'ombre du Tout-Puissant.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
Je dis à l'Éternel: «Tu es mon refuge et ma forteresse, Mon Dieu en qui je mets ma confiance!»
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
C'est lui qui te délivrera du filet de l'oiseleur Et de la peste meurtrière.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Il te couvrira de ses ailes. Et sous sa protection tu trouveras un refuge; Sa fidélité sera ton bouclier protecteur.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Tu ne craindras ni les terreurs de la nuit. Ni la flèche qui vole pendant le jour,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Ni la peste qui se glisse à travers les ténèbres, Ni la mortalité qui sévit en plein midi.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Quand il tomberait mille hommes à ton côté Et dix mille à ta droite. Tu ne serais pas atteint.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Mais toi, tu contempleras de tes yeux Et tu verras le châtiment des méchants.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Oui, tu es mon refuge, ô Éternel! Tu as pris le Très-Haut pour ton asile.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Aucun mal ne t'atteindra; Aucun fléau n'approchera de ta tente.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
Car il ordonnera à ses anges De te garder dans toutes tes entreprises.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
Ils te porteront sur leurs mains, De peur que ton pied ne heurte contre une pierre.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Tu marcheras sur le lion et sur l'aspic; Tu écraseras le lionceau et le dragon.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
«Puisqu'il s'est attaché à moi, je le délivrerai; Je le mettrai en sûreté, puisqu'il connaît mon nom.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Il m'invoquera, et je l'exaucerai; Je serai avec lui dans la détresse, Je l'en retirerai et je le glorifierai.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Je le rassasierai de longs jours. Et je lui ferai contempler mon salut.»

< Zaburi 91 >