< Zaburi 91 >
1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Celui qui demeure sous la sauvegarde du Très-Haut, et s’abrite à l’ombre du Tout-Puissant,
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
qu’il dise à l’Eternel: "Tu es mon refuge, ma citadelle, mon Dieu, en qui je place ma confiance!"
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
Car c’est lui qui te préserve du piège de l’oiseleur, de la peste meurtrière.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Il te recouvre de ses vastes pennes; sous ses ailes tu trouves un refuge: sa bonté est un bouclier et une cuirasse.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Tu n’auras à craindre ni les terreurs de la nuit, ni les flèches qui voltigent le jour,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
ni la peste qui chemine dans l’ombre, ni l’épidémie qui exerce ses ravages en plein midi.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Qu’à tes côtés il en tombe mille, dix mille à ta droite: toi, le mal ne t’atteindra point.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Tu le verras seulement de tes yeux, tu seras témoin de la rémunération des méchants.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
C’Est que tu as dit: "L’Eternel est mon refuge!" Dans le Très-Haut tu as placé ton abri.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Nul malheur ne te surviendra, nul fléau n’approchera de ta tente;
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
car à ses anges il a donné mission de te protéger en toutes tes voies.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
Sur leurs bras ils te porteront, pour que ton pied ne se heurte à aucune pierre.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Tu marcheras sur le chacal et la vipère, tu fouleras le lionceau et le serpent.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
"Car dit le Seigneur il m’est attaché, et je veux le sauver du danger; je veux le grandir, parce qu’il connaît mon nom.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Il m’appelle et je lui réponds; je suis avec lui dans la détresse, je le délivre et le comble d’honneur.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Je le rassasie de longs jours, et le fais jouir de mon salut.