< Zaburi 91 >
1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
He that dwelleth in the secret place of the Most High, Under the shadow of the Almighty, will tarry,
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
Saying of Yahweh—My refuge and my fortress, My God, in whom I will trust.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For, he, will rescue thee, From the snare of the fowler, From the destructive pestilence.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
With his pinion, will he cover thee, And, under his wings, shalt thou seek refuge, A shield and buckler, is his faithfulness.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Thou shalt not be afraid, Of the dread of the night, Of the arrow that flieth by day;
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Of the pestilence that, in darkness, doth walk, Of the plague that layeth waste at noonday.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
There shall fall, at thy side, a thousand, Yea, myriads, at thy right hand, Unto thee, shall it not come nigh;
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Save only, with thine own eyes, shalt thou discern, And, the recompense of the lawless, shalt thou see.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Because, thou, [hast made] Yahweh, my refuge, —The Most High, thou hast made thy dwelling-place,
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
There shall not be sent unto thee misfortune, Nor shall, plague, come near into thy tent;
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For, his messengers, will he charge concerning thee, To keep thee, in all thy ways;
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
On hands, will they bear thee up, Lest thou strike, against a stone, thy foot;
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
On the lion and adder, shalt thou tread, Shalt trample on young lion and crocodile.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Because, on me, he hath set firm his love, Therefore will I deliver him, I will set him on high, Because he hath known my Name;
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He shall call me, and I will answer him, With him, will, I, be, in distress, I will rescue him, and will honour him;
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
With length of days, will I satisfy him, And will show him my salvation.