< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
The praise of a canticle for David. He that dwelleth in the aid of the most High, shall abide under the protection of the God of Jacob.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
He shall say to the Lord: Thou art my protector, and my refuge: my God, in him will I trust.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For he hath delivered me from the snare of the hunters: and from the sharp word.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
He will overshadow thee with his shoulders: and under his wings thou shalt trust.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
His truth shall compass thee with a shield: thou shalt not be afraid of the terror of the night.
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Of the arrow that flieth in the day, of the business that walketh about in the dark: of invasion, or of the noonday devil.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand shall fall at thy side, and ten thousand at thy right hand: but it shall not come nigh thee.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
But thou shalt consider with thy eyes: and shalt see the reward of the wicked.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Because thou, O Lord, art my hope: thou hast made the most High thy refuge.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
There shall no evil come to thee: nor shall the scourge come near thy dwelling.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For he hath given his angels charge over thee; to keep thee in all thy ways.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
In their hands they shall bear thee up: lest thou dash thy foot against a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Thou shalt walk upon the asp and the basilisk: and thou shalt trample under foot the lion and the dragon.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Because he hoped in me I will deliver him: I will protect him because he hath known my name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He shall cry to me, and I will hear him: I am with him in tribulation, I will deliver him, and I will glorify him.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
I will fill him with length of days; and I will shew him my salvation.

< Zaburi 91 >