< Zaburi 91 >
1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
The Praise of a Canticle, of David. Whoever dwells with the assistance of the Most High will abide in the protection of the God of heaven.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
He will say to the Lord, “You are my supporter and my refuge.” My God, I will hope in him.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For he has freed me from the snare of those who go hunting, and from the harsh word.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
He will overshadow you with his shoulders, and you will hope under his wings.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
His truth will surround you with a shield. You will not be afraid: before the terror of the night,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
before the arrow flying in the day, before the troubles that wander in the darkness, nor of invasion and the midday demon.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand will fall before your side and ten thousand before your right hand. Yet it will not draw near you.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
So then, truly, you will consider with your eyes, and you will see the retribution of sinners.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
For you, O Lord, are my hope. You have set the Most High as your refuge.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Disaster will not draw near to you, and the scourge will not approach your tabernacle.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For he has given his Angels charge over you, so as to preserve you in all your ways.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
With their hands, they will carry you, lest you hurt your foot against a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
You will walk over the asp and the king serpent, and you will trample the lion and the dragon.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Because he has hoped in me, I will free him. I will protect him because he has known my name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He will cry out to me, and I will heed him. I am with him in tribulation. I will rescue him, and I will glorify him.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
I will fill him with length of days. And I will reveal to him my salvation.