< Zaburi 88 >

1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
Una canción. Un salmo de los descendientes de Coré. Para el director del coro. Al son de “Mahalath Leannoth”. Un masquil por Hemán el ezraíta Señor, Dios de mi salvación, clamo a ti de día y de noche.
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
Por favor escucha mi oración; escucha mis palabras de súplica.
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
Mi vida está llena de problemas, y mi muerte se acerca. (Sheol h7585)
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
Soy contado entre los moribundos; un hombre sin fuerzas.
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
Soy abandonado entre los muertos, tendido como un cadáver en la tumba, olvidado y dejado a tu cuidado.
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
Me has puesto en un pozo profundo, entre las penumbras.
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
Tu hostilidad me maltrata; me estás ahogando entre tus olas abrumadoras. (Selah)
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
Has hecho que mis enemigos me eviten, haciéndome repulsivo a sus vistas. Estoy atrapado, no puedo huir.
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
Señor, he llorado suplicándote cada día por ayuda, extendiendo mis manos hacia ti.
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
¿Haces milagros entre los muertos? ¿Se levantan los muertos para alabarte? (Selah)
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
Tu gran amor, ¿Se menciona en la tumba? Tu fidelidad, ¿Es discutida en lugar de destrucción?
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
¿Las cosas maravillosas que haces son conocidas en las tinieblas? ¿Tu bondad es conocida en la tierra del olvido?
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
Pero clamo a ti pidiendo ayuda; cada mañana oro a ti.
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
Señor, ¿Por qué me rechazas? ¿Por qué te alejas de mí?
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
He estado enfermo desde que era joven, a menudo estuve a las puertas de la muerte. He tenido que soportar las cosas terribles que me has hecho. ¡Estoy desesperado!
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
Tu ira me ha vencido; las cosas terribles que haces me han destruido.
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
Ellos me rodean constantemente como aguas de una inundación, succionándome.
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
Has hecho que mi familia y mis amigos se alejen. La oscuridad es mi única amiga.

< Zaburi 88 >