< Zaburi 88 >

1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
canticum psalmi filiis Core in finem pro Maeleth ad respondendum intellectus Eman Ezraitae Domine Deus salutis meae die clamavi et nocte coram te
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
intret in conspectu tuo oratio mea inclina aurem tuam ad precem meam
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
quia repleta est malis anima mea et vita mea in inferno adpropinquavit (Sheol h7585)
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
aestimatus sum cum descendentibus in lacum factus sum sicut homo sine adiutorio
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
inter mortuos liber sicut vulnerati dormientes in sepulchris quorum non es memor amplius et ipsi de manu tua repulsi sunt
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
posuerunt me in lacu inferiori in tenebrosis et in umbra mortis
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
super me confirmatus est furor tuus et omnes fluctus tuos induxisti super me diapsalma
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
longe fecisti notos meos a me posuerunt me abominationem sibi traditus sum et non egrediebar
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
oculi mei languerunt prae inopia clamavi ad te Domine tota die expandi ad te manus meas
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
numquid mortuis facies mirabilia aut medici suscitabunt et confitebuntur tibi diapsalma
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
numquid narrabit aliquis in sepulchro misericordiam tuam et veritatem tuam in perditione
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
numquid cognoscentur in tenebris mirabilia tua et iustitia tua in terra oblivionis
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
et ego ad te Domine clamavi et mane oratio mea praeveniet te
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
ut quid Domine repellis orationem meam avertis faciem tuam a me
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
pauper sum ego et in laboribus a iuventute mea exaltatus autem humiliatus sum et conturbatus
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
in me transierunt irae tuae et terrores tui conturbaverunt me
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
circuierunt me sicut aqua tota die circumdederunt me simul
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
elongasti a me amicum et proximum et notos meos a miseria

< Zaburi 88 >