< Zaburi 88 >
1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
Une chanson. Un psaume par les fils de Korah. Pour le chef musicien. Sur l'air de « The Suffering of Affliction ». Une contemplation par Heman, l'Ezrahite. Yahvé, le Dieu de mon salut, J'ai pleuré jour et nuit devant vous.
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
Que ma prière entre en ta présence. Prêtez l'oreille à mon cri.
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol )
Car mon âme est pleine d'angoisse. Ma vie s'approche du séjour des morts. (Sheol )
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
Je suis compté parmi ceux qui descendent dans la fosse. Je suis comme un homme qui n'a pas d'aide,
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
mis à part parmi les morts, comme les morts qui reposent dans la tombe, dont vous ne vous souvenez plus. Ils sont coupés de ta main.
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
Tu m'as déposé dans la fosse la plus profonde, dans les profondeurs les plus sombres.
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
Ta colère pèse sur moi. Tu m'as affligé de toutes tes vagues. (Selah)
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
Tu m'as enlevé mes amis. Tu as fait de moi une abomination pour eux. Je suis confiné, et je ne peux pas m'échapper.
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
Mes yeux s'assombrissent à cause du chagrin. Je t'ai invoqué chaque jour, Yahvé. J'ai tendu mes mains vers vous.
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
Faites-vous des prodiges aux morts? Est-ce que les esprits défunts se lèvent et vous louent? (Selah)
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
Ta bonté est-elle déclarée dans la tombe? Ou votre fidélité dans la Destruction?
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
Tes merveilles se font-elles connaître dans l'obscurité? Ou ta justice dans le pays de l'oubli?
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
Mais c'est à toi, Yahvé, que j'ai crié. Le matin, ma prière vient devant vous.
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
Yahvé, pourquoi rejettes-tu mon âme? Pourquoi me cachez-vous votre visage?
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
Je suis affligé et prêt à mourir depuis ma jeunesse. Pendant que je souffre de tes terreurs, je suis distrait.
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
Ton ardente colère s'est abattue sur moi. Vos terreurs m'ont coupé.
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
Ils m'ont entouré comme de l'eau toute la journée. Ils m'ont complètement englouti.
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
Tu as éloigné de moi l'amant et l'ami, et mes amis dans les ténèbres.