< Zaburi 88 >
1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
song melody to/for son: descendant/people Korah to/for to conduct upon Mahalath to/for to sing Maskil to/for Heman [the] Ezrahite LORD God salvation my day to cry in/on/with night before you
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
to come (in): come to/for face: before your prayer my to stretch ear your to/for cry my
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol )
for to satisfy in/on/with distress: harm soul my and life my to/for hell: Sheol to touch (Sheol )
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
to devise: count with to go down pit to be like/as great man nothing strength
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
in/on/with to die free like slain: killed to lie down: be dead grave which not to remember them still and they(masc.) from hand your to cut
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
to set: put me in/on/with pit lower in/on/with darkness in/on/with depth
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
upon me to support rage your and all wave your to afflict (Selah)
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
to remove to know my from me to set: make me abomination to/for them to restrain and not to come out: come
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
eye my to languish from affliction to call: call to you LORD in/on/with all day to spread to(wards) you palm my
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
to/for to die to make: do wonder if: surely no shade to arise: rise to give thanks you (Selah)
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
to recount in/on/with grave kindness your faithfulness your in/on/with Abaddon
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
to know in/on/with darkness wonder your and righteousness your in/on/with land: country/planet forgetfulness
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
and I to(wards) you LORD to cry and in/on/with morning prayer my to meet you
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
to/for what? LORD to reject soul my to hide face your from me
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
afflicted I and to die from youth to lift: bear terror your to distract
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
upon me to pass burning anger your terror your to destroy me
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
to turn: surround me like/as water all [the] day to surround upon me unitedness
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
to remove from me to love: lover and neighbor to know my darkness