< Zaburi 88 >

1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
A song of a Psalm for the sons of Core for the end, upon Maeleth for responsive [strains], of instruction for Aeman the Israelite. O Lord God of my salvation, I have cried by day and in the night before thee.
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
Let my prayer come in before thee; incline thine ear to my supplication, O Lord.
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
For my soul is filled with troubles, and my life has drawn nigh to Hades. (Sheol h7585)
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
I have been reckoned with them that go down to the pit; I became as a man without help;
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
free among the dead, as the slain ones cast out, who sleep in the tomb; whom thou rememberest no more; and they are rejected from thy hand.
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
They laid me in the lowest pit, in dark [places], and in the shadow of death.
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
Thy wrath has pressed heavily upon me, and thou hast brought upon me all thy billows. (Pause)
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
Thou hast removed my acquaintance far from me; they have made me an abomination to themselves; I have been delivered up, and have not gone forth.
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
Mine eyes are dimmed from poverty; but I cried to thee, O Lord, all the day; I spread forth my hands to thee.
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
Wilt thou work wonders for the dead? or shall physicians raise [them] up, that they shall praise thee?
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
Shall any one declare thy mercy in the tomb? and thy truth in destruction?
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
Shall thy wonders be known in darkness? and thy righteousness in a forgotten land?
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
But I cried to thee, O Lord; and in the morning shall my prayer prevent thee.
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
Wherefore, O Lord, dost thou reject my prayer, [and] turn thy face away from me?
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
I am poor and in troubles from my youth; and having been exalted, I was brought low and into despair.
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
Thy wrath has passed over me; and thy terrors have greatly disquieted me.
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
They compassed me like water; all the day they beset me together.
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
Thou hast put far from me [every] friend, and mine acquaintances because of [my] wretchedness.

< Zaburi 88 >