< Zaburi 87 >
1 Mji aliouanzisha umesimama juu ya mlima mtakatifu;
A Psalm of a Song for the sons of Core. His foundations are in the holy mountains.
2 Yahwe anapenda zaidi malango ya Sayuni kuliko mahema yote ya Yakobo.
The Lord loves the gates of Sion, more than all the tabernacles of Jacob.
3 Mambo matukufu yamesemwa kwako, mji wa Mungu. (Selah)
Glorious things have been spoken of you, O city of God. (Pause)
4 Ninataja Rahabu na Babeli kwa wafuasi wangu. Tazama, Filisti, na Tiro, pamoja na Ethiopia nao watasema, 'Huyu alizaliwa humo.'”
I will make mention of Raab and Babylon to them that know me: behold also the Philistines, and Tyre, and the people of the Ethiopians: these were born there.
5 Itasemwa juu ya Sayuni, “Kila mmoja wa hawa alizaliwa katika yeye; na yeye Aliye Juu atamuimarisha.
A man shall say, Sion [is my] mother; and [such] a man was born in her; and the Highest himself has founded her.
6 Yahwe anaandika katika kitabau cha sensa ya mataifa, “Huyu alizaliwa humo.” (Selah)
The Lord shall recount [it] in the writing of the people, and of these princes that were born in her.
7 Hivyo waimbaji na wachezaji kwa pamoja waseme, “chemchem zangu zimo kwako.”
The dwelling of all within you is [as the dwelling] of those that rejoice.