< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Señor, fuiste bueno con tu tierra: cambiando el destino de Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
La maldad de tu pueblo tuvo perdón; todos sus pecados cubriste. (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Ya no estabas enojado: fuiste apartado del ardor de tu ira.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Regresa a nosotros, oh Dios de nuestra salvación, y no te enojes más con nosotros.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
¿Seguirás enojado con nosotros para siempre? ¿guardarás tu ira contra nosotros a lo largo de todas las generaciones?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
¿No nos darás la vida otra vez, para que tu pueblo se alegre en ti?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Veamos tu misericordia, Señor, y danos tu salvación.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
Oiré la voz del Señor; porque él dirá palabras de paz a su pueblo y a sus santos; pero que no vuelvan a sus maneras necias.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Verdaderamente, su salvación está cerca de sus adoradores; para que la gloria esté en nuestra tierra.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
La misericordia y la fe se han unido; la justicia y la paz se han dado un beso.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
La fe sube de la tierra como una planta; la justicia está mirando hacia abajo desde el cielo.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
El Señor dará lo que es bueno; y nuestra tierra dará su fruto.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
La justicia irá delante de él, haciendo un camino para sus pasos.

< Zaburi 85 >