< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Dem Vorsänger. Von den Kindern Korahs. Ein Psalm. HERR, du warst einst gnädig deinem Land, hast das Gefängnis Jakobs gewendet,
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
vergabst deines Volkes Schuld, decktest alle ihre Sünden zu, (Pause)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
du ließest ab von deinem Grimm, wandtest dich von deines Zornes Glut:
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Stelle uns wieder her, o Gott unsres Heils, laß ab von deinem Grimm gegen uns!
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Oder willst du ewig mit uns zürnen, deinen Zorn währen lassen von Geschlecht zu Geschlecht?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Willst du uns nicht wieder neu beleben, daß dein Volk sich deiner freuen kann?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
HERR, laß uns deine Gnade schauen und schenke uns dein Heil!
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
Ich will hören, was Gott, der HERR, reden wird; denn er wird Frieden zusagen seinem Volk und seinen Frommen. Nur daß sie sich nicht wieder zur Torheit wenden!
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Gewiß ist sein Heil denen nahe, die ihn fürchten, daß Herrlichkeit in unserm Lande wohne,
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
daß Gnade und Wahrheit einander begegnen, Gerechtigkeit und Friede sich küssen,
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
daß Treue aus der Erde sprieße und Gerechtigkeit vom Himmel schaue.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Der HERR wird uns auch Gutes geben, und unser Land wird seinen Ertrag abwerfen;
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Gerechtigkeit wird vor ihm hergehen und ihre Füße setzen auf den Pfad.

< Zaburi 85 >