< Zaburi 85 >
1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Auf den Siegesspender, von den Korachiten, ein Lied. Du hast Dein Land begnadet, Herr, und Jakobs Schicksal umgewandelt,
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
vergeben Deines Volkes Schuld, bedeckt all ihr Vergehen. (Sela)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Du zogst all Deinen Grimm zurück und dämpftest Deine Zornesglut.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Du, unser hilfereicher Gott, geh weiterhin mit uns! Und tilge vollends Deinen Unmut wider uns!
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Willst Du denn ewig auf uns zürnen, auf alle Zeiten Deinen Zorn ausdehnen?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Willst Du uns nicht aufs neu beleben, auf daß Dein Volk sich Deiner freue?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Erzeig uns Deine Gnade, Herr! Gewähre uns Dein Heil! -
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
Ich möchte hören, was der Herr verheißt: Er spricht von Frieden für sein Volk und seine Frommen, für die, die umkehren, von Hoffnung.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Schon naht sein Heil sich denen, die ihn fürchten, auf daß die Herrlichkeit in unserm Lande wieder wohne.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Dann finden sich die Liebe und die Treue; Gerechtigkeit und Frieden küssen sich.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Die Treue reckt auf Erden sich, und die Gerechtigkeit neigt sich vom Himmel.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Der Herr beschert alsdann den Segen, und unser Land gibt seine volle Ernte wieder.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Gerechtigkeit geht vor ihm her, und auf dem Wege seiner Schritte ist Geradheit.