< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Au maître de chant. Psaume des fils de Coré. Tu as été favorable à ton pays, Yahweh, tu as ramené les captifs de Jacob;
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
tu as pardonné l’iniquité à ton peuple, tu as couvert tous ses péchés; — Séla.
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
tu as retiré toute ton indignation, tu es revenu de l’ardeur de ta colère.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Rétablis-nous, Dieu de notre salut; mets fin à ton sentiment contre nous.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Seras-tu toujours irrité contre nous, prolongeras-tu ton courroux éternellement?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Ne nous feras-tu pas revenir à la vie, afin que ton peuple se réjouisse en toi?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Yahweh, fais-nous voir ta bonté, et accorde-nous ton salut.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
Je veux écouter ce que dira le Dieu Yahweh: — Il a des paroles de paix pour son peuple et pour ses fidèles; pourvu qu’ils ne retournent pas à leur folie. —
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Oui, son salut est proche de ceux qui le craignent, et la gloire habitera de nouveau dans notre pays.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
La bonté et la vérité vont se rencontrer, la justice et la paix s’embrasseront.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
La vérité germera de la terre, et la justice regardera du haut du ciel.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Yahweh lui-même accordera tout bien, et notre terre donnera son fruit.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
La justice marchera devant lui, et tracera le chemin à ses pas.

< Zaburi 85 >