< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Pour le chef musicien. Un psaume par les fils de Korah. Yahvé, tu as été favorable à ton pays. Vous avez restauré la fortune de Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
Tu as pardonné l'iniquité de ton peuple. Tu as couvert tous leurs péchés. (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Tu as ôté toute ta colère. Tu t'es détourné de l'ardeur de ta colère.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Tourne-nous, Dieu de notre salut, et fais cesser ton indignation à notre égard.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Seras-tu toujours en colère contre nous? Voulez-vous étendre votre colère à toutes les générations?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Ne nous ranimeras-tu pas encore, pour que ton peuple se réjouisse en toi?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Montre-nous ta bonté, Yahvé. Accorde-nous ton salut.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
J'écouterai ce que Dieu, Yahvé, dira, car il parlera de paix à son peuple, ses saints; mais qu'ils ne se tournent pas à nouveau vers la folie.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Son salut est proche de ceux qui le craignent, pour que la gloire habite dans notre pays.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
La miséricorde et la vérité se rencontrent. La justice et la paix se sont embrassées.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
La vérité jaillit de la terre. La justice a regardé du haut des cieux.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Oui, Yahvé donnera ce qui est bon. Notre terre donnera ses fruits.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
La justice le précède, et prépare le chemin pour ses pas.

< Zaburi 85 >