< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
For the chief musician. A psalm of the sons of Korah. Yahweh, you have showed favor to your land; you have restored the well-being of Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
You have forgiven the sin of your people; you have covered all their sin. (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
You have withdrawn all your wrath; you have turned back from your hot anger.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Restore us, God of our salvation, and let go of your displeasure with us.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Will you be angry with us forever? Will you remain angry throughout future generations?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Will you not revive us again? Then your people will rejoice in you.
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Show us your covenant faithfulness, Yahweh, grant us your salvation.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
I will listen to what Yahweh God says, for he will make peace with his people, his faithful followers. Yet they must not turn again to foolish ways.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Surely his salvation is near to those who fear him; then glory will remain in our land.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Covenant faithfulness and trustworthiness have met together; righteousness and peace have kissed each other.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Trustworthiness springs up from the ground, and righteousness looks down from the sky.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Yes, Yahweh will give his good blessings, and our land will yield its crops.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Righteousness will go before him and make a way for his footsteps.

< Zaburi 85 >