< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
To the choirmaster - of [the] sons of Korah a psalm. You showed favor to O Yahweh land your you turned back ([the] captivity of *Q(k)*) Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
You forgave [the] iniquity of people your you covered all sin their (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
You withdrew all fury your you turned back from [the] burning of anger your.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Restore us O God of salvation our and break anger your with us.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
¿ To forever will you be angry with us will you prolong? anger your to a generation and a generation.
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
¿ Not you will you return will you give life? us and people your they will rejoice in you.
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Show us O Yahweh covenant loyalty your and salvation your you will give to us.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
I will listen to whatever he will say God - Yahweh for - he will speak peace to people his and to faithful [people] his and may not they return to folly.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Surely - [is] near to [those] fearing him salvation his to dwell glory in land our.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Covenant loyalty and faithfulness they meet together righteousness and peace they kiss.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Faithfulness from [the] earth it springs up and righteousness from heaven it looks down.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Also Yahweh he will give the good and land our it will give produce its.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Righteousness before him it will go and it will make to [the] way of footsteps his.

< Zaburi 85 >