< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Unto the end, for the sons of Core, a psalm. Lord, thou hast blessed thy land: thou hast turned away the captivity of Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
Thou hast forgiven the iniquity of thy people: thou hast covered all their sins.
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Thou hast mitigated all thy anger: thou best turned away from the wrath of thy indignation.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Convert us, O God our saviour: and turn off thy anger from us.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Wilt thou be angry with us for ever: or wilt thou extend thy wrath from generation to generation?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Thou wilt turn, O God, and bring us to life: and thy people shall rejoice in thee.
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Shew us, O Lord, thy mercy; and grant us thy salvation.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
I will hear what the Lord God will speak in me: for he will speak peace unto his people: And unto his saints: and unto them that are converted to the heart.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Surely his salvation is near to them that fear him: that glory may dwell in our land.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Mercy and truth have met each other: justice and peace have kissed.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Truth is sprung out of the earth: and justice hath looked down from heaven.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
For the Lord will give goodness: and our earth shall yield her fruit.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Justice shall walk before him: and shall set his steps in the way.

< Zaburi 85 >