< Zaburi 85 >
1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
To the chief music-maker. A Psalm. Of the sons of Korah. Lord, you were good to your land: changing the fate of Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
The wrongdoing of your people had forgiveness; all their sin had been covered. (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
You were no longer angry: you were turned from the heat of your wrath.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Come back to us, O God of our salvation, and be angry with us no longer.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Will you go on being angry with us for ever? will you keep your wrath against us through all the long generations?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Will you not give us life again, so that your people may be glad in you?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Let us see your mercy, O Lord, and give us your salvation.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
I will give ear to the voice of the Lord; for he will say words of peace to his people and to his saints; but let them not go back to their foolish ways.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Truly, his salvation is near to his worshippers; so that glory may be in our land.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Mercy and faith have come together; righteousness and peace have given one another a kiss.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Faith comes up from the earth like a plant; righteousness is looking down from heaven.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
The Lord will give what is good; and our land will give its increase.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Righteousness will go before him, making a way for his footsteps.