< Zaburi 85 >
1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Jehovah, thou have been favorable to thy land. Thou have brought back the captivity of Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
Thou have forgiven the iniquity of thy people. Thou have covered all their sin. (Selah)
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Thou have taken away all thy wrath. Thou have turned from the fierceness of thine anger.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Turn us, O God of our salvation, and cause thine indignation toward us to cease.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
Will thou be angry with us forever? Will thou draw out thine anger to all generations?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
Will thou not revive us again, that thy people may rejoice in thee?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Show us thy loving kindness, O Jehovah, and grant us thy salvation.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
I will hear what God, Jehovah, will speak, for he will speak peace to his people, and to his sanctified. But let them not turn again to folly.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Surely his salvation is near those who fear him, that glory may dwell in our land.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
Mercy and truth are met together. Righteousness and peace have kissed each other.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
Truth springs out of the earth, and righteousness has looked down from heaven.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
Yea, Jehovah will give that which is good, and our land shall yield its increase.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
Righteousness shall go before him, and shall make his footsteps a path.