< Zaburi 83 >
1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
canticum psalmi Asaph Deus quis similis erit tibi ne taceas neque conpescaris Deus
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
quoniam ecce inimici tui sonaverunt et qui oderunt te extulerunt caput
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
super populum tuum malignaverunt consilium et cogitaverunt adversus sanctos tuos
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
dixerunt venite et disperdamus eos de gente et non memoretur nomen Israhel ultra
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
quoniam cogitaverunt unianimiter simul adversum te testamentum disposuerunt
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
tabernacula Idumeorum et Ismahelitae Moab et Aggareni
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
Gebal et Ammon et Amalech alienigenae cum habitantibus Tyrum
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
etenim Assur venit cum illis facti sunt in adiutorium filiis Loth diapsalma
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
fac illis sicut Madiam et Sisarae sicut Iabin in torrente Cison
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
disperierunt in Endor facti sunt ut stercus terrae
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
pone principes eorum sicut Oreb et Zeb et Zebee et Salmana omnes principes eorum
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
qui dixerunt hereditate possideamus sanctuarium Dei
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
Deus meus pone illos ut rotam sicut stipulam ante faciem venti
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
sicut ignis qui conburit silvam sicut flamma conburens montes
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
ita persequeris illos in tempestate tua et in ira tua turbabis eos
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
imple facies illorum ignominia et quaerent nomen tuum Domine
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
erubescant et conturbentur in saeculum saeculi et confundantur et pereant
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
et cognoscant quia nomen tibi Dominus tu solus Altissimus in omni terra