< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
アサフの歌、さんび 神よ、沈黙を守らないでください。神よ、何も言わずに、黙っていないでください。
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
見よ、あなたの敵は騒ぎたち、あなたを憎む者は頭をあげました。
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
彼らはあなたの民にむかって巧みなはかりごとをめぐらし、あなたの保護される者にむかって相ともに計ります。
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
彼らは言います、「さあ、彼らを断ち滅ぼして国を立てさせず、イスラエルの名をふたたび思い出させないようにしよう」。
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
彼らは心をひとつにして共にはかり、あなたに逆らって契約を結びます。
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
すなわちエドムの天幕に住む者とイシマエルびと、モアブとハガルびと、
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
ゲバルとアンモンとアマレク、ペリシテとツロの住民などです。
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
アッスリヤもまた彼らにくみしました。彼らはロトの子孫を助けました。 (セラ)
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
あなたがミデアンにされたように、キション川でシセラとヤビンにされたように、彼らにしてください。
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
彼らはエンドルで滅ぼされ、地のために肥料となりました。
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
彼らの貴人をオレブとゼエブのように、そのすべての君たちをゼバとザルムンナのようにしてください。
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
彼らは言いました、「われらは神の牧場を獲て、われらの所有にしよう」と。
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
わが神よ、彼らを巻きあげられるちりのように、風の前のもみがらのようにしてください。
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
林を焼く火のように、山を燃やす炎のように、
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
あなたのはやてをもって彼らを追い、つむじかぜをもって彼らを恐れさせてください。
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
彼らの顔に恥を満たしてください。主よ、そうすれば彼らはあなたの名を求めるでしょう。
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
彼らをとこしえに恥じ恐れさせ、あわて惑って滅びうせさせてください。
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
主という名をおもちになるあなたのみ、全地をしろしめすいと高き者であることを彼らに知らせてください。

< Zaburi 83 >