< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
Ein Psalmlied Asaphs. Gott, schweige doch nicht also und sei doch nicht so still; Gott, halt doch nicht so inne!
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
Denn siehe, deine Feinde toben, und die dich hassen, richten den Kopf auf.
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
Sie machen listige Anschläge gegen dein Volk und ratschlagen wider deine Verborgenen.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
“Wohl her!” sprechen sie; “laßt uns sie ausrotten, daß sie kein Volk seien, daß des Namens Israel nicht mehr gedacht werde!”
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
Denn sie haben sich miteinander vereinigt und einen Bund wider dich gemacht,
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
die Hütten der Edomiter und Ismaeliter, der Moabiter und Hagariter,
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
der Gebaliter, Ammoniter und Amalekiter, die Philister samt denen zu Tyrus;
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
Assur hat sich auch zu ihnen geschlagen; sie helfen den Kindern Lot. (Sela)
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Tue ihnen, wie den Midianitern, wie Sisera, wie Jabin am Bach Kison,
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
die vertilgt wurden bei Endor und wurden zu Kot auf der Erde.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Mache ihre Fürsten wie Oreb und Seeb, alle ihre Obersten wie Sebah und Zalmuna,
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
die da sagen: Wir wollen Häuser Gottes einnehmen.
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
Gott, mache sie wie einen Wirbel, wie Stoppeln vor dem Winde.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
Wie ein Feuer den Wald verbrennt und wie eine Flamme die Berge anzündet:
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
also verfolge sie mit deinem Wetter und erschrecke sie mit deinem Ungewitter.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Mache ihr Angesicht voll Schande, daß sie nach deinem Namen fragen müssen, o HERR.
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Schämen müssen sie sich und erschrecken auf immer und zu Schanden werden und umkommen;
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
so werden sie erkennen, daß du mit deinem Namen heißest HERR allein und der Höchste in aller Welt.

< Zaburi 83 >