< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
God, don’t keep silent. Don’t keep silent, and don’t be still, God.
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
For, behold, your enemies are stirred up. Those who hate you have lifted up their heads.
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
They conspire with cunning against your people. They plot against your cherished ones.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
“Come,” they say, “let’s destroy them as a nation, that the name of Israel [God prevails] may be remembered no more.”
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
For they have conspired together with one mind. They form an alliance against you.
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
The tents of Edom [Red] and the Ishmaelites [Pays attention God]; Moab [From father], and the Hagrites;
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
Gebal, Ammon [Tribal people], and Amalek [Man who licks up]; Philistia with the inhabitants of Tyre;
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
Assyria [Level plain] also is joined with them. They have helped the children of Lot [Veil, Covering]. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Do to them as you did to Midian [Strife], as to Sisera, as to Jabin, at the river Kishon;
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
who perished at Endor, who became as dung for the earth.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Make their nobles like Oreb and Zeeb; yes, all their princes like Zebah and Zalmunna;
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
who said, “Let us take possession of God’s pasture lands.”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
My God, make them like tumbleweed; like chaff before the wind.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
As the fire that burns the forest, as the flame that sets the mountains on fire,
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
so pursue them with your tempest, and terrify them with your storm.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Fill their faces with confusion, that they may seek your name, Adonai.
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Let them be disappointed and dismayed forever. Yes, let them be confounded and perish;
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
that they may know that you alone, whose name is Adonai, are haElyon [the Most High] over all the earth.

< Zaburi 83 >