< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
A Song, a Psalm of Asaph. O God, keep not Thou silence; hold not Thy peace, and be not still, O God.
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
For, lo, Thine enemies are in an uproar; and they that hate Thee have lifted up the head.
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
They hold crafty converse against Thy people, and take counsel against Thy treasured ones.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
They have said: 'Come, and let us cut them off from being a nation; that the name of Israel may be no more in remembrance.'
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
For they have consulted together with one consent; against Thee do they make a covenant;
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
The tents of Edom and the Ishmaelites; Moab, and the Hagrites;
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
Gebal, and Ammon, and Amalek; Philistia with the inhabitants of Tyre;
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
Assyria also is joined with them; they have been an arm to the children of Lot. (Selah)
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Do Thou unto them as unto Midian; as to Sisera, as to Jabin, at the brook Kishon;
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
Who were destroyed at En-dor; they became as dung for the earth.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Make their nobles like Oreb and Zeeb, and like Zebah and Zalmunna all their princes;
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
Who said: 'Let us take to ourselves in possession the habitations of God.'
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
O my God, make them like the whirling dust; as stubble before the wind.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
As the fire that burneth the forest, and as the flame that setteth the mountains ablaze;
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
So pursue them with Thy tempest, and affright them with Thy storm.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Fill their faces with shame; that they may seek Thy name, O LORD.
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Let them be ashamed and affrighted for ever; yea, let them be abashed and perish;
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
That they may know that it is Thou alone whose name is the LORD, the Most High over all the earth.

< Zaburi 83 >