< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
A song. A psalm of Asaph. God, please do not stay silent! You can't remain unmoved! God, you must not keep quiet!
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
Can't you hear the roars of your enemies? Can't you see how those who hate you are defiantly lifting up their heads?
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
They invent cunning plans to conspire against your people; they plot against those you treasure.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
They say, “Come on! Let's destroy them as a nation so the name ‘Israel’ will be completely forgotten.”
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
They all agree in their conspiracy; they've made a treaty together to attack you—
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
the people of Edom, the Ishmaelites, Moab, and the Hagirites;
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
the people of Gebal and Ammon and Amalek, Philistia, and the inhabitants of Tyre.
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
Assyria too has joined them, allied with the descendants of Lot. (Selah)
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Do to them what you did to Midian, what you did to Sisera and Jabin at the Kishon River.
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
They were destroyed at Endor and became like manure to fertilize the ground.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Make their leaders like Oreb and Zeeb; all their rulers like Zebah and Zalmunna,
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
for they said, “Let's take the pastures of God for ourselves!”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
My God, make them like whirling tumbleweeds, chaff blown away by the wind.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
Just like fire that burns the forest, a flame that sets fire to the mountains,
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
in the same way chase them down with your storm, terrify them with your whirlwind.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Shame them in defeat so that they come to you, Lord!
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Make them ashamed, terrify them forever so that they die in disgrace.
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
Let them understand that you alone, called the Lord, are the Most High who rules over all the earth.

< Zaburi 83 >