< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
A canticle of a psalm for Asaph. O God, who shall be like to thee? hold not thy peace, neither be thou still, O God.
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
For lo, thy enemies have made a noise: and they that hate thee have lifted up the head.
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
They have taken a malicious counsel against thy people, and have consulted against thy saints.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
They have said: Come and let us destroy them, so that they be not a nation: and let the name of Israel be remembered no more.
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
For they have contrived with one consent: they have made a covenant together against thee,
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
The tabernacles of the Edomites, and the Ismahelites: Moab, and the Agarens,
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
Gebal, and Ammon and Amalec: the Philistines, with the inhabitants of Tyre.
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
Yea, and the Assyrian also is joined with them: they are come to the aid of the sons of Lot.
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Do to them as thou didst to Madian and to Sisara: as to Jabin at the brook of Cisson.
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
Who perished at Endor: and became as dung for the earth.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Make their princes like Oreb, and Zeb, and Zebee, and Salmana. All their princes,
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
Who have said: Let us possess the sanctuary of God for an inheritance.
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
O my God, make them like a wheel; and as stubble before the wind.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
As fire which burneth the wood: and as a flame burning mountains:
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
So shalt thou pursue them with thy tempest: and shalt trouble them in thy wrath.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Fill their faces with shame; and they shall seek thy name, O Lord.
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Let them be ashamed and troubled for ever and ever: and let them be confounded and perish.
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
And let them know that the Lord is thy name: thou alone art the most High over all the earth.

< Zaburi 83 >