< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
詠【求消滅聯盟的異民】阿撒夫的詩歌。 上主,求您不要一言不發,天主,您們不要靜默無話!
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
因為您的仇敵騷擾狂吼,惱恨您的人都搖頭昂首;
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
相聚密謀,陷害您的百姓,商議攻擊您保護的人民,
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
說:大家來,由萬民將要他們驅散,使以色列的名不再被記念。
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
於是,他們心齊謀同,締結盟約,向您進攻,
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
即厄東部落及依市瑪耳,又有摩阿布以及哈革爾。
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
還有革巴耳、阿孟和阿瑪肋克人,且有培肋舍特人和提洛的居民,
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
亞述人也與他們串通,作了羅特子民的幫兇。
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
求你對待他們像對待米德楊人,像在克雄河對待息色辣和雅賓,
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
他們都喪亡於恩多爾,全變成了田裏的糞泥,
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
使他們的王侯要與敖勒布和東一樣,使他們的將領與巴黑和匝耳慕一樣,
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
因為他們都曾如此說過:我們去佔領天主的住所。
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
我的天主,求您使他們像旋風捲起的落葉,求您使他們像狂風吹起的碎楷,
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
好像被火燐焚燒的樹林,又似被火燄燃燒的山陵;
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
求您也這樣以您的颶風驅散他們,以您的暴雨驚嚇他們。
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
上主,求您羞辱他們的面容,是為叫他們尋求您的聖名;
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
使他們永遠受辱恐慌,叫他們個個蒙羞喪亡。
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
從此,認識您的名號是雅威,惟有您在普天下至尊無對。

< Zaburi 83 >