< Zaburi 82 >
1 Mungu amesimama katika kusanyiko la mbinguni; katikati ya miungu anahukumu.
アサフの歌 神は神の会議のなかに立たれる。神は神々のなかで、さばきを行われる。
2 Hata lini mtahukumu bila haki na kuonesha upendeleo kwa waovu? (Selah)
「あなたがたはいつまで不正なさばきをなし、悪しき者に好意を示すのか。 (セラ)
3 Wateteeni maskini na yatima; dumisheni haki kwa aliyetaabishwa na fukara.
弱い者と、みなしごとを公平に扱い、苦しむ者と乏しい者の権利を擁護せよ。
4 Muokoeni maskini na muhitaji; watoeni mkononi mwa waovu.
弱い者と貧しい者を救い、彼らを悪しき者の手から助け出せ」。
5 Hawajui wala hawaelewi; hutembea gizani; misingi yote ya nchi imebomoka.
彼らは知ることなく、悟ることもなくて、暗き中をさまよう。地のもろもろの基はゆり動いた。
6 Mimi nilisema, “Ninyi ni miungu, na ninyi nyote wana wa Mungu aliye Juu.
わたしは言う、「あなたがたは神だ、あなたがたは皆いと高き者の子だ。
7 Hata hivyo mtakufa kama wanadamu na mtaanguka kama mmoja wa wakuu.”
しかし、あなたがたは人のように死に、もろもろの君のひとりのように倒れるであろう」。
8 Uinuke, Ee Mungu, uihukumu nchi, maana unaurithi katika mataifa yote.
神よ、起きて、地をさばいてください。すべての国民はあなたのものだからです。