< Zaburi 81 >

1 Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
in finem pro torcularibus Asaph exultate Deo adiutori nostro iubilate Deo Iacob
2 Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
sumite psalmum et date tympanum psalterium iucundum cum cithara
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
bucinate in neomenia tuba in insigni die sollemnitatis nostrae
4 Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
quia praeceptum Israhel est et iudicium Dei Iacob
5 Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
testimonium in Ioseph posuit illud cum exiret de terra Aegypti linguam quam non noverat audivit
6 “Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
devertit ab oneribus dorsum eius manus eius in cofino servierunt
7 Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
in tribulatione invocasti me et liberavi te exaudivi te in abscondito tempestatis probavi te apud aquam Contradictionis diapsalma
8 Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
audi populus meus et contestabor te Israhel si audias me
9 Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
non erit in te deus recens nec adorabis deum alienum
10 Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
ego enim sum Dominus Deus tuus qui eduxi te de terra Aegypti dilata os tuum et implebo illud
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
et non audivit populus meus vocem meam et Israhel non intendit mihi
12 Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
et dimisi illos secundum desideria cordis eorum ibunt in adinventionibus suis
13 Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
si populus meus audisset me Israhel si in viis meis ambulasset
14 Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
pro nihilo forsitan inimicos eorum humiliassem et super tribulantes eos misissem manum meam
15 Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
inimici Domini mentiti sunt ei et erit tempus eorum in saeculo
16 Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”
et cibavit illos ex adipe frumenti et de petra melle saturavit illos

< Zaburi 81 >