< Zaburi 81 >

1 Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
Sing [songs] to praise God, who enables us to be strong [when we fight our enemies]; shout joyfully to God, whom we (descendants of Jacob/Israeli people) [worship]!
2 Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
Start [playing] the music, and beat the tambourines, and play nice music on the harps and (lyres/other stringed instruments).
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
Blow the trumpets [during the festival to celebrate] each new moon and each time the moon is full and during our [other] festivals.
4 Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
[Do that] because that is a law for [us] Israeli [people]; God commanded it for us descendants of Jacob.
5 Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
He commanded us Israeli [people to obey it] when he punished [the people of] Egypt. I heard someone [MTY] whose voice I did not recognize, saying,
6 “Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
“[After the rulers of Egypt forced you Israelis to work as slaves], I took those [heavy] burdens off your backs, and I enabled you to lay down those [heavy] baskets [of bricks that you were carrying].
7 Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
When you were [greatly] distressed, you called [out to me], and I rescued you; I answered you out of a thundercloud. [Later] I tested [whether you would trust me to give you] water [when you were in the desert] at Meribah.
8 Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
[You who are] my people, listen while I warn you! I wish that you Israeli [people] would pay attention to what I [say to you]!
9 Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
You must not have any idols of other gods among you; you must never bow to worship any of them!
10 Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
I am Yahweh, your God; It was [not any of those other gods] who brought you out of Egypt, I am the one who did it! [So] ask me what you want me to do for you [MTY], and I will do it.
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
But my people would not listen to me [SYN]; they would not obey me.
12 Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
So even though they were very stubborn, I allowed them to do whatever they wanted to do.
13 Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
I wish that my people would listen to me, that the Israeli [people] would behave as I want them to do.
14 Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
[If they did that], I would quickly defeat their enemies; I would strike/punish [all of] them [DOU].
15 Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
[Then all] those who hate me would (cringe before/bow down to) me, and [then I] would punish them [MTY] forever.
16 Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”
[But] I would give you [Israelis] very good wheat/grain, and I would fill your stomachs with wild honey.”

< Zaburi 81 >