< Zaburi 81 >

1 Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
To the chief Musician upon Gittith, [A Psalm] of Asaph. Sing aloud unto God our strength: make a joyful noise unto the God of Jacob.
2 Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
Take a psalm, and bring hither the timbrel, the pleasant harp with the psaltery.
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
Blow up the trumpet in the new moon, in the time appointed, on our solemn feast day.
4 Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
For this [was] a statute for Israel, [and] a law of the God of Jacob.
5 Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
This he ordained in Joseph [for] a testimony, when he went out through the land of Egypt: [where] I heard a language [that] I understood not.
6 “Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
I removed his shoulder from the burden: his hands were delivered from the pots.
7 Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
Thou calledst in trouble, and I delivered thee; I answered thee in the secret place of thunder: I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
8 Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
Hear, O my people, and I will testify unto thee: O Israel, if thou wilt hearken unto me;
9 Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
There shall no strange god be in thee; neither shalt thou worship any strange god.
10 Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
I [am] the LORD thy God, which brought thee out of the land of Egypt: open thy mouth wide, and I will fill it.
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
But my people would not hearken to my voice; and Israel would none of me.
12 Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
So I gave them up unto their own hearts’ lust: [and] they walked in their own counsels.
13 Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
Oh that my people had hearkened unto me, [and] Israel had walked in my ways!
14 Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
I should soon have subdued their enemies, and turned my hand against their adversaries.
15 Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
The haters of the LORD should have submitted themselves unto him: but their time should have endured for ever.
16 Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”
He should have fed them also with the finest of the wheat: and with honey out of the rock should I have satisfied thee.

< Zaburi 81 >