< Zaburi 81 >

1 Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
Unto the end. For the wine and oil presses. A Psalm of Asaph himself. Exult before God our helper. Sing joyfully to the God of Jacob.
2 Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
Take up a psalm, and bring forth the timbrel: a pleasing Psalter with stringed instruments.
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
Sound the trumpet at the new moon, on the noteworthy day of your solemnity,
4 Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
for it is a precept in Israel and a judgment for the God of Jacob.
5 Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
He set it as a testimony with Joseph, when he went out of the land of Egypt. He heard a tongue that he did not know.
6 “Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
He turned the burdens away from his back. His hands had been a slave to baskets.
7 Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
You called upon me in tribulation, and I freed you. I heard you within the hidden tempest. I tested you with waters of contradiction.
8 Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
My people, listen and I will call you to testify. If, O Israel, you will pay heed to me,
9 Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
then there will be no new god among you, nor will you adore a foreign god.
10 Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
For I am the Lord your God, who led you out of the land of Egypt. Widen your mouth, and I will fill it.
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
But my people did not hear my voice, and Israel was not attentive to me.
12 Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
And so, I sent them away, according to the desires of their heart. They will go forth according to their own inventions.
13 Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
If my people had heard me, if Israel had walked in my ways,
14 Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
I would have humbled their enemies, as if it were nothing, and I would have sent my hand upon those who troubled them.
15 Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
The enemies of the Lord have lied to him, and their time will come, in every age.
16 Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”
And he fed them from the fat of the grain, and he saturated them with honey from the rock.

< Zaburi 81 >