< Zaburi 80 >
1 Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
Give ear, O Shepherd of Israel, you that lead Joseph like a flock; you that dwell between the cherubims, shine forth.
2 Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Manasseh stir up your strength, and come and save us.
3 Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
Turn us again, O God, and cause your face to shine; and we shall be saved.
4 Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
O LORD God of hosts, how long will you be angry against the prayer of your people?
5 Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
You feed them with the bread of tears; and give them tears to drink in great measure.
6 Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
You make us a strife unto our neighbours: and our enemies laugh among themselves.
7 Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
Turn us again, O God of hosts, and cause your face to shine; and we shall be saved.
8 Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
You have brought a vine out of Egypt: you have cast out the heathen, and planted it.
9 Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
You prepared room before it, and did cause it to take deep root, and it filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
The hills were covered with the shadow of it, and the boughs thereof were like the goodly cedars.
11 Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
She sent out her boughs unto the sea, and her branches unto the river.
12 Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
Why have you then broken down her hedges, so that all they which pass by the way do pluck her?
13 Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
The boar out of the wood does waste it, and the wild beast of the field does devour it.
14 Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
Return, we plead to you, O God of hosts: look down from heaven, and behold, and visit this vine;
15 Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
And the vineyard which your right hand has planted, and the branch that you made strong for yourself.
16 Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
It is burned with fire, it is cut down: they perish at the rebuke of your countenance.
17 Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
Let your hand be upon the man of your right hand, upon the son of man whom you made strong for yourself.
18 Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
So will not we go back from you: quicken us, and we will call upon your name.
19 Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.
Turn us again, O LORD God of hosts, cause your face to shine; and we shall be saved.