< Zaburi 80 >

1 Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
For the choirmaster. To the tune of “The Lilies of the Covenant.” A Psalm of Asaph. Hear us, O Shepherd of Israel, who leads Joseph like a flock; You who sit enthroned between the cherubim, shine forth
2 Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
before Ephraim, Benjamin, and Manasseh. Rally Your mighty power and come to save us.
3 Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
Restore us, O God, and cause Your face to shine upon us, that we may be saved.
4 Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
O LORD God of Hosts, how long will Your anger smolder against the prayers of Your people?
5 Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
You fed them with the bread of tears and made them drink the full measure of their tears.
6 Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
You make us contend with our neighbors; our enemies mock us.
7 Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
Restore us, O God of Hosts, and cause Your face to shine upon us, that we may be saved.
8 Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
You uprooted a vine from Egypt; You drove out the nations and transplanted it.
9 Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
You cleared the ground for it, and it took root and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
The mountains were covered by its shade, and the mighty cedars with its branches.
11 Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
It sent out its branches to the Sea, and its shoots toward the River.
12 Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
Why have You broken down its walls, so that all who pass by pick its fruit?
13 Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
The boar from the forest ravages it, and the creatures of the field feed upon it.
14 Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
Return, O God of Hosts, we pray! Look down from heaven and see! Attend to this vine—
15 Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
the root Your right hand has planted, the son You have raised up for Yourself.
16 Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
Your vine has been cut down and burned; they perish at the rebuke of Your countenance.
17 Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
Let Your hand be upon the man at Your right hand, on the son of man You have raised up for Yourself.
18 Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
Then we will not turn away from You; revive us, and we will call on Your name.
19 Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.
Restore us, O LORD God of Hosts; cause Your face to shine upon us, that we may be saved.

< Zaburi 80 >