< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
in finem pro torcularibus psalmus David Domine Dominus noster quam admirabile est nomen tuum in universa terra quoniam elevata est magnificentia tua super caelos
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
ex ore infantium et lactantium perfecisti laudem propter inimicos tuos ut destruas inimicum et ultorem
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
quoniam videbo caelos tuos; opera digitorum tuorum lunam et stellas quae tu fundasti
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
quid est homo quod memor es eius aut filius hominis quoniam visitas eum
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
minuisti eum paulo minus ab angelis gloria et honore coronasti eum
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
et constituisti eum super opera manuum tuarum
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
omnia subiecisti sub pedibus eius oves et boves universas insuper et pecora campi
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
volucres caeli et pisces maris qui perambulant semitas maris
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
Domine Dominus noster quam admirabile est nomen tuum in universa terra

< Zaburi 8 >