< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
(다윗의 시. 영장으로 깃딧에 맞춘 노래) 여호와 우리 주여, 주의 이름이 온 땅에 어찌 그리 아름다운지요 주의 영광을 하늘 위에 두셨나이다
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
주의 대적을 인하여 어린 아이와 젖먹이의 입으로 말미암아 권능을 세우심이여 이는 원수와 보수자로 잠잠케 하려 하심이니이다
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
주의 손가락으로 만드신 주의 하늘과 주의 베풀어 두신 달과 별들을 내가 보오니
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
사람이 무엇이관대 주께서 저를 권고하시나이까
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
저를 천사보다 조금 못하게 하시고 영화와 존귀로 관을 씌우셨나이다
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
주의 손으로 만드신 것을 다스리게 하시고 만물을 그 발 아래 두셨으니
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
곧 모든 우양과 들짐승이며
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
여호와 우리 주여, 주의 이름이 온 땅에 어찌 그리 아름다운지요

< Zaburi 8 >