< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
Yahweh, our Lord, people all over the world know that you [MTY] are very great! Your glory reaches up higher than the heavens!
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
You have taught little children and infants to praise you; they cause your enemies and those who try to (get revenge on/get rid of) you to be silent.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
When I look up at the sky [at night], and see the things that you have made— the moon and the stars that you have set in place—
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
it is amazing [to me] that [RHQ] you think about people, that you are concerned about [us] humans!
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
You made the angels in heaven to be only a little more important than we are; you caused us to be like kings [MET] and you gave us splendor and honor [DOU]!
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
You put us in charge of everything that you made; you gave us authority over all things—
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
the sheep and the cattle, and even the wild animals,
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
the birds, the fish, and everything [else] that swims in the seas.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
Yahweh, our Lord, people all over the world know that you [MTY] are very great!

< Zaburi 8 >