< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
Adonai, our Lord, how majestic is your name in all the earth, who has set your glory above the heavens!
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
From the lips of babes and infants you have established strength, because of your adversaries, that you might silence the enemy and the avenger.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
When I consider your heavens, the work of your fingers, the moon and the stars, which you have ordained;
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
what is man, that you think of him? What is the son of man, that you care for him?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
For you have made him a little lower than the angels, and crowned him with glory and honor.
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
You make him ruler over the works of your hands. You have put all things under his feet:
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
All sheep and cattle, yes, and the animals of the field,
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
The birds of the sky, the fish of the sea, and whatever passes through the paths of the seas.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
Adonai, our Lord, how majestic is your name in all the earth!

< Zaburi 8 >