< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
To him that excelleth on Gittith. A Psalme of Dauid. O Lord our Lord, how excellent is thy Name in all the worlde! which hast set thy glory aboue the heauens.
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
Out of the mouth of babes and suckelings hast thou ordeined strength, because of thine enemies, that thou mightest still the enemie and the auenger.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
When I beholde thine heauens, euen the workes of thy fingers, the moone and the starres which thou hast ordeined,
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
What is man, say I, that thou art mindefull of him? and the sonne of man, that thou visitest him?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
For thou hast made him a little lower then God, and crowned him with glory and worship.
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
Thou hast made him to haue dominion in the workes of thine hands: thou hast put all things vnder his feete:
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
All sheepe and oxen: yea, and the beastes of the fielde:
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
The foules of the ayre, and the fish of the sea, and that which passeth through the paths of the seas.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
O Lord our Lord, howe excellent is thy Name in all the world!

< Zaburi 8 >