< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
For the end, concerning the wine-presses, a Psalm of David. O Lord, our Lord, how wonderful is thy name in all the earth! for thy magnificence is exalted above the heavens.
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
Out of the mouth of babes and sucklings hast thou perfected praise, because of thine enemies; that thou mightest put down the enemy and avenger.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
For I will regard the heavens, the work of thy fingers; the moon and stars, which thou hast established.
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
What is man, that thou art mindful of him? or the son of man, that thou visitest him?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
Thou madest him a little less than angels, thou hast crowned him with glory and honour;
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
and thou hast set him over the works of thy hands: thou hast put all things under his feet:
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
sheep and all oxen, yea and the cattle of the field;
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
the birds of the sky, and the fish of the sea, the [creatures] passing through the paths of the sea.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
O Lord our Lord, how wonderful is thy name in all the earth!

< Zaburi 8 >