< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
For the choirmaster. According to Gittith. A Psalm of David. O LORD, our Lord, how majestic is Your name in all the earth! You have set Your glory above the heavens.
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
From the mouths of children and infants You have ordained praise on account of Your adversaries, to silence the enemy and avenger.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
When I behold Your heavens, the work of Your fingers, the moon and the stars, which You have set in place—
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
what is man that You are mindful of him, or the son of man that You care for him?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
You made him a little lower than the angels; You crowned him with glory and honor.
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
You made him ruler of the works of Your hands; You have placed everything under his feet:
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
all sheep and oxen, and even the beasts of the field,
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
the birds of the air and the fish of the sea, all that swim the paths of the seas.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
O LORD, our Lord, how majestic is Your name in all the earth!

< Zaburi 8 >