< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Masquil de Asaf. Escucha, pueblo mío, mi ley; inclinad vuestro oído a las palabras de mi boca.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Abriré mi boca en parábola; hablaré enigmas del tiempo antiguo.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Las cuales hemos oído y entendido; que nuestros padres nos las contaron.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
No las encubriremos a sus hijos, contando a la generación venidera las alabanzas del SEÑOR, y su fortaleza, y sus maravillas que hizo.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
El estableció testimonio en Jacob, y puso ley en Israel; las cuales mandó a nuestros padres que las notificasen a sus hijos;
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
para que lo sepa la generación venidera, y los hijos que nacerán; y los que se levantarán, lo cuenten a sus hijos
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
con el fin de poner su confianza en Dios, y no olvidar de las obras de Dios, y guardar sus mandamientos:
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Y no ser como sus padres, generación contumaz y rebelde; generación que no compuso su corazón, ni su espíritu fue fiel con Dios.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Los hijos de Efraín armados, flecheros, volvieron las espaldas el día de la batalla.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
No guardaron el pacto de Dios, ni quisieron andar en su ley;
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
antes se olvidaron de sus obras, y de sus maravillas que les había mostrado.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Delante de sus padres hizo maravillas en la tierra de Egipto, en el campo de Zoán.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Rompió el mar, y los hizo pasar; e hizo estar las aguas como en un montón.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Y los llevó con nube de día, y toda la noche con resplandor de fuego.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Hendió las peñas en el desierto; y les dio a beber de abismos grandes;
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
y sacó de la peña corrientes, e hizo descender aguas como ríos.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Pero aun tornaron a pecar contra él, enojando al Altísimo en la soledad.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Y tentaron a Dios en su corazón, pidiendo comida al gusto de su alma.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Y hablaron contra Dios, diciendo: ¿Podrá Dios ponernos mesa en el desierto?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
He aquí ha herido la peña, y corrieron aguas, y arroyos salieron ondeando: ¿Podrá también dar pan? ¿Aparejará carne a su pueblo?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Por tanto oyó el SEÑOR, y se enojó; se encendió el fuego contra Jacob, y el furor subió también contra Israel;
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
por cuanto no habían creído a Dios, ni habían confiado de su salud.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Y mandó a las nubes de arriba, y abrió las puertas de los cielos,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
e hizo llover sobre ellos maná para comer, y les dio trigo de los cielos.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Pan de fuertes comió el hombre; les envió comida en abundancia.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Movió el solano en el cielo, y trajo con su fortaleza el austro,
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
e hizo llover sobre ellos carne como polvo, y aves de alas como arena del mar.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Y las hizo caer en medio de su campamento, alrededor de sus tiendas.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Y comieron, y se llenaron bien; les cumplió pues su deseo.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
No habían quitado de sí su deseo, aun estaba su vianda en su boca,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
cuando vino sobre ellos el furor de Dios, y mató los más robustos de ellos, y derribó los escogidos de Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Con todo esto pecaron aún, y no dieron crédito a sus maravillas.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Consumió por tanto sus días en vanidad, y sus años en tribulación.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Si los mataba, entonces le buscaban; y se convertían, y buscaban a Dios de mañana.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Y se acordaban que Dios era su refugio, y el Dios Alto su redentor.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Mas le lisonjeaban con su boca, y con su lengua le mentían,
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
pues sus corazones no eran rectos con él, ni estuvieron firmes en su pacto.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Pero él, misericordioso, perdonaba la maldad, y no los destruyó; y abundó su misericordia para apartar su ira, y no despertó toda su ira.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Y se acordó que eran carne; soplo que va y no vuelve.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
¡Cuántas veces lo ensañaron en el desierto, lo enojaron en la soledad!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Y volvían, y tentaban a Dios, y ponían límite al Santo de Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
No se acordaron de su mano, del día que los redimió de angustia;
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
cuando puso en Egipto sus señales, y sus maravillas en el campo de Zoán;
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
y volvió sus ríos en sangre, y sus corrientes para que no bebiesen.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Envió entre ellos enjambres de moscas que los comían, y ranas que los destruyeron.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Dio también al pulgón sus frutos, y sus trabajos a la langosta.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Sus viñas destruyó con granizo, y sus higuerales con piedra;
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
y entregó al pedrisco sus bestias, y al fuego sus ganados.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Envió sobre ellos el furor de su saña; ira, enojo, angustia, y ángeles malos.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Dispuso el camino a su furor; no eximió el alma de ellos de la muerte, sino que entregó su vida a la mortandad.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
E hirió a todo primogénito en Egipto, las primicias de las fuerzas en las tiendas de Cam.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Hizo salir a su pueblo como ovejas, y los llevó por el desierto, como un rebaño.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Y los pastoreó con seguridad, que no tuvieron miedo; y el mar cubrió a sus enemigos.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Los metió después en los términos de su santidad, en este monte que ganó su mano derecha.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Y echó los gentiles de delante de ellos, y les repartió una herencia con cuerdas; e hizo habitar en sus moradas a las tribus de Israel.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Mas tentaron y enojaron al Dios Altísimo, y no guardaron sus testimonios;
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
sino que se volvieron, y se rebelaron como sus padres; se volvieron como arco engañoso.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Y le enojaron con sus lugares altos, y le provocaron a celo con sus esculturas.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Lo oyó Dios, y se enojó, y en gran manera aborreció a Israel.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Por esta causa dejó el tabernáculo de Silo, la tienda en que habitó entre los hombres;
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
y dio en cautividad su fortaleza, y su gloria en mano del enemigo.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Entregó también su pueblo a cuchillo, y se airó contra su heredad.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
El fuego devoró sus jóvenes, y sus vírgenes no fueron loadas en cantos nupciales.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Sus sacerdotes cayeron a cuchillo, y sus viudas no se lamentaron.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Entonces despertó el Señor a la manera del que ha dormido, como un valiente que grita a causa del vino:
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
e hirió a sus enemigos en las partes posteriores; les dio perpetua afrenta.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Y aborreció la tienda de José, y no escogió la tribu de Efraín.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Sino que escogió la tribu de Judá, el monte de Sion, al cual amó.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Y edificó su santuario a manera de eminencia, como la tierra que cimentó para siempre.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Y eligió a David su siervo, y lo tomó de las majadas de las ovejas;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
de tras las paridas lo trajo, para que apacentase a Jacob su pueblo, y a Israel su heredad.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Y los apacentó con entereza de su corazón; y los pastoreó con la pericia de sus manos.