< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Una contemplación de Asaf. Escuchad mi enseñanza, pueblo mío. Vuelve tus oídos a las palabras de mi boca.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Voy a abrir mi boca en una parábola. Pronunciaré oscuros refranes de antaño,
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
que hemos oído y conocido, y nuestros padres nos lo han dicho.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
No los esconderemos de sus hijos, contar a la generación venidera las alabanzas de Yahvé, su fuerza y las maravillas que ha hecho.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Porque estableció un pacto en Jacob, y designó una enseñanza en Israel, que ordenó a nuestros padres, que los den a conocer a sus hijos;
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
para que la generación venidera lo sepa, incluso los niños que han de nacer; que deben levantarse y decírselo a sus hijos,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
para que pongan su esperanza en Dios, y no olvidar las obras de Dios, sino que guarden sus mandamientos,
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
y que no sean como sus padres — una generación obstinada y rebelde, una generación que no ha fidelizado su corazón, cuyo espíritu no estaba firme con Dios.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Los hijos de Efraín, armados y con arcos, se volvió atrás en el día de la batalla.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
No cumplieron el pacto de Dios, y se negó a caminar en su ley.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Se olvidaron de sus actos, sus maravillosas hazañas que les había mostrado.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Hizo cosas maravillosas a la vista de sus padres, en la tierra de Egipto, en el campo de Zoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Partió el mar y los hizo pasar. Hizo que las aguas se mantuvieran como un montón.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
De día también los guiaba con una nube, y toda la noche con una luz de fuego.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Partió rocas en el desierto, y les dio de beber abundantemente como de las profundidades.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
También sacó arroyos de la roca, e hizo que las aguas corrieran como ríos.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Sin embargo, siguieron pecando contra él, para rebelarse contra el Altísimo en el desierto.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Tentaron a Dios en su corazón pidiendo comida según su deseo.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Sí, hablaron contra Dios. Dijeron: “¿Puede Dios preparar una mesa en el desierto?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
He aquí que golpeó la roca, de modo que las aguas brotaron, y los arroyos se desbordaron. ¿Puede dar pan también? ¿Proporcionará carne a su pueblo?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Por lo tanto, Yahvé escuchó y se enojó. Se encendió un fuego contra Jacob, La ira también se dirigió contra Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
porque no creían en Dios, y no confió en su salvación.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Sin embargo, él mandaba en los cielos, y abrió las puertas del cielo.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
Hizo llover maná sobre ellos para que comieran, y les dio comida del cielo.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
El hombre comió el pan de los ángeles. Les mandó comida hasta la saciedad.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Hizo que el viento del este soplara en el cielo. Con su poder guió el viento del sur.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
También hizo llover sobre ellos carne como el polvo, aves aladas como la arena de los mares.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Los dejó caer en medio de su campamento, alrededor de sus viviendas.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Comieron, pues, y se saciaron. Les dio su propio deseo.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
No se apartaron de sus antojos. La comida aún estaba en sus bocas,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
cuando la ira de Dios subió contra ellos, mató a algunos de sus más fuertes, y abatió a los jóvenes de Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
A pesar de todo esto, pecaron, y no creían en sus maravillosas obras.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Por eso consumió sus días en la vanidad, y sus años de terror.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Cuando los mató, entonces preguntaron por él. Volvieron y buscaron a Dios con ahínco.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Recordaron que Dios era su roca, el Dios Altísimo, su redentor.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Pero ellos lo halagaron con su boca, y le mintieron con la lengua.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Porque su corazón no estaba bien con él, ni fueron fieles a su pacto.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Pero él, siendo misericordioso, perdonó la iniquidad y no los destruyó. Sí, muchas veces desvió su ira, y no despertó toda su ira.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Recordó que no eran más que carne, un viento que pasa y no vuelve.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Cuántas veces se rebelaron contra él en el desierto, ¡y lo afligió en el desierto!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Se volvieron y tentaron a Dios, y provocó al Santo de Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
No se acordaron de su mano, ni el día en que los redimió del adversario;
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
cómo puso sus signos en Egipto, sus maravillas en el campo de Zoan,
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
convirtió sus ríos en sangre, y sus arroyos, para que no pudieran beber.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Envió entre ellos enjambres de moscas, que los devoraron; y ranas, que los destruyeron.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
También le dio su aumento a la oruga, y su trabajo a la langosta.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Destruyó sus vides con el granizo, sus higueras de sicomoro con la escarcha.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
También entregó su ganado al granizo, y sus rebaños a los rayos calientes.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Arrojó sobre ellos la ferocidad de su ira, la ira, la indignación y los problemas, y una banda de ángeles del mal.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Hizo un camino para su ira. No les perdonó el alma de la muerte, sino que entregaron su vida a la peste,
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
y golpeó a todos los primogénitos de Egipto, el jefe de su fuerza en las tiendas de Cam.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Pero sacó a los suyos como a ovejas, y los guió en el desierto como un rebaño.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Los condujo con seguridad, para que no tuvieran miedo, pero el mar arrolló a sus enemigos.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Los llevó a la frontera de su santuario, a esta montaña, que su mano derecha había tomado.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
También expulsó a las naciones que estaban delante de ellos, les asignó una herencia por línea, e hizo que las tribus de Israel habitasen en sus tiendas.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Sin embargo, tentaron y se rebelaron contra el Dios Altísimo, y no mantuvo sus testimonios,
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
sino que se volvieron atrás, y actuaron con traición como sus padres. Estaban retorcidos como un arco engañoso.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Porque lo provocaron a la ira con sus lugares altos, y lo movieron a los celos con sus imágenes grabadas.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Cuando Dios escuchó esto, se enojó, y aborrecía enormemente a Israel,
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
por lo que abandonó la tienda de Silo, la tienda que colocó entre los hombres,
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
y entregó su fuerza al cautiverio, su gloria en la mano del adversario.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
También entregó a su pueblo a la espada, y se enfadó con su herencia.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
El fuego devoró a sus jóvenes. Sus vírgenes no tenían canción de boda.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Sus sacerdotes cayeron por la espada, y sus viudas no podían llorar.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Entonces el Señor se despertó como quien sale del sueño, como un hombre poderoso que grita a causa del vino.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Golpeó a sus adversarios hacia atrás. Los sometió a un reproche perpetuo.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Además, rechazó la tienda de José, y no eligió la tribu de Efraín,
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Pero eligió la tribu de Judá, El Monte Sión que él amaba.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Construyó su santuario como las alturas, como la tierra que ha establecido para siempre.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
También eligió a David, su siervo, y lo sacaron de los rediles;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
de seguir a las ovejas que tienen sus crías, lo llevó a ser el pastor de Jacob, su pueblo, e Israel, su herencia.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Así quefue su pastor según la integridad de su corazón, y los guió con la destreza de sus manos.

< Zaburi 78 >