< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Un salmo (masquil) de Asaf. Escucha, pueblo mío, lo que tengo para enseñarte. Escucha lo que vengo a decirte.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Te enseñaré dichos sabios; y te explicaré misterios del pasado
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
que he escuchado antes y sobre los cuales he reflexionado. Son historias de nuestros antepasados que han sido transmitidas por generaciones.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
No las ocultaremos de nuestros hijos. Le contaremos a la siguiente generación sobre las maravillas que Dios ha hecho; sobre su poder y grandes obras.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Él entregó sus leyes a los descendientes de Jacob; dio sus instrucciones al pueblo de Israel. Él ordenó a nuestros padres para que las enseñaran a sus hijos,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
a fin de que la siguiente generación—los que aún no habían nacido—entendieran y crecieran para enseñar a sus hijos.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
De esta forma debían mantener su fe en Dios y no olvidar lo que Dios ha hecho, así como seguir sus mandamientos.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Para que no fueran como sus antepasados, una generación terca y rebelde que carecía de fe y fidelidad.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Los soldados de Efraín, aunque estaban armados con arcos, huyeron el día de la batalla.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
No cumplieron el pacto de Dios, y se negaron a seguir sus leyes.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Ignoraronl lo que Dios había hecho, y las maravillas que les había mostrado antes:
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
los milagros que había hecho por sus antepasados en Zoán, en Egipto.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Él dividió el mar en dos y los condujo a través de él, manteniendo las aguas como muros a cada lado.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Él los guiaba con una nube en el día, y de noche con una nube de fuego.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Partió las rocas en el desierto para darle agua abundante a su pueblo. Aguas profundas como el océano.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
¡Él hizo que de las piedras fluyera agua como un río!
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Pero ellos siguieron pecando contra él, rebelándose contra el Altísimo mientras andaban por el desierto.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Deliberadamente provocaban a Dios, exigiendo las comidas que tanto anhelaban.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Insultaron a Dios diciendo: “¿Puede Dios darnos comida aquí en el desierto?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Si bien puede golpear una roca y hacer que de ellas fluya agua como corrientes de río, ¿puede acaso darnos pan? ¿Puede darnos carne?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Cuando el Señor oyó esto, se enojó mucho, y el fuego de su enojo se encendió contra los descendientes de Jacob, el pueblo de Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
porque ellos no creyeron en Dios y no confiaron en que podía cuidar de ellos.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Tanto fue su enojo que ordenó a los cielos se abrieran,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
e hizo llover maná del cielo, dándoles así pan celestial.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Los seres humanos comieron del pan que comen los ángeles. Y les dio más que suficiente.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Luego hizo soplar un viento desde el Este, y por su poder también hizo soplar el viento que viene del Sur.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Hizo llover carne como tan abundante como el polvo. Las aves eran muchas, como la arena de la playa.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
E hizo caer las aves en medio del campamento, y alrededor de sus carpas.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Y comieron hasta que se saciaron. Les dio la comida que tanto deseaban.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Pero antes de saciar su apetito, mientras aún masticaban la carne,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
Dios se enojó con ellos e hizo morir a los hombres más fuertes, derribándolos en plena juventud.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
A pesar de esto, siguieron pecando. A pesar de los milagros, se negaban a creer en él.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Así que apagó sus vidas vanas, e hizo que terminaran sus años con horror.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Cuando Dios comenzó a matarlos, volvieron con oraciones a él, arrepentidos de su pecado.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Se acordaron de que Dios era su roca, que el Dios Altísimo era su salvador.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Entonces lo comenzaron adular de labios para afuera, pero solo mentían.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
En sus corazones no eran sinceros y no guardaron el pacto que tenían con él.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Pero por su compasión él perdonó su pecado y no los destruyó. Muchas veces contuvo su enojo y no desató toda su furia.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Dios recordó que eran simples mortales, y que eran como el viento que se va y no regresa.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Cuántas veces se rebelaron contra él en el desierto, causándole tristeza.
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Una y otra vez provocaron a Dios, causando dolor al Santo de Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Olvidaron la fuerza con la que él los rescató de sus opresores,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
haciendo milagros en Egipto, y maravillas en la llanura de Zoán.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Allí convirtió sus ríos y fuentes de agua en sangre, de modo que nadie podía beber de ellos.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Envió moscas para destruirlos, y ranas para que los arruinaran.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Dio sus cultivos a las langostas, y todo el fruto de su trabajo fue devorado por ellas.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Destruyó sus viñedos con granizo, y sus higueras con aguanieve.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Dejó su ganado a merced del granizo y sus animales fueron destruidos por relámpagos.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Envió sobre ellos su ira feroz: Rabia, hostilidad y agonía. Por ello envió un grupo de ángeles destructores.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Desató su ira sobre ellos y no los salvó de la muerte, sino que los dejó morir por causa de esta plaga.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
Entonces mató al hijo mayor de cada familia en Egipto, todos los que habían sido concebidos como primogénitos en las carpas de Ham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Pero a su pueblo guió como ovejas, y los condujo como un rebaño en el desierto.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Los llevó a un lugar seguro, y no tuvieron nada que temer. Ahogó a sus enemigos en el mar.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Los llevó hasta la frontera de su tierra santa, a esta tierra montañosa que había conquistado para ellos.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
A las naciones infieles las expulsaba a su paso. Dividió la tierra para que la hicieran suya. Estableció las tribus de Israel en sus carpas.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Pero ellos siguieron provocando al Altísimo, siendo rebeldes contra él. No siguieron sus enseñanzas.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Así como sus antiguos padres se alejaron de Dios y fueron infieles a él, tan torcidos como un arco doblado que no sirve.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Provocaron su ira con sus altares paganos y despertaron su celo con sus ídolos.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Cuando Dios escuchó que adoraban a otros dioses se enfureció y rechazó por completo a Israel.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Entonces abandonó su lugar en Siloé, el Tabernáculo en el que vivía en medio del pueblo.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Además entregó el arca de su poder, dejando que manos enemigas la tomaran.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Entregó a su pueblo y permitió que lo masacraran a espada, pues estaba furioso con su pueblo escogido.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Sus hombres más jóvenes fueron quemados, y las mujeres jóvenes no lograron cantar sus cánticos de bodas.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Sus sacerdotes fueron asesinados con espadas y sus viudas no pudieron hacer duelo por ellos.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Entonces el Señor reaccionó como si hubiera despertado del sueño, como un guerrero que se despierta después de embriagarse con vino.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Venció a sus enemigos, atacándolos por la espalda y exponiéndolos a vergüenza eterna.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Rechazó a los descendientes de José y no elegió más a la tribu de Eraín.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
En su lugar eligió a la tribu de Judá y al Monte de Sión, al cual amaba.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Allí construyó su santuario, tan alto como el cielo, y lo puso allí en esa tierra para que existiera eternamente.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Eligió a su siervo David, tomándolo de entre los rediles de ovejas,
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
y lo llevó de cuidar ovejas y corderos, a ser un pastor de los descendientes de Jacob, el pueblo especial de Dios: Israel.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Como un pastor cuidó de ellos con sincera devoción, y los condujo con manos hábiles.